Monday, June 7, 2010

KIKWETE NDANI YA MOSHI LEO KWA ZIARA YA SIKU 3

Rais Jakaya kikwete leo anafanya ziara kwa mara nyingine tena mkoani kilimanjaro, ambapo atazindua tawi jipya la benki ya biashara la Kenya –KBC,lililopo mjini moshi.


Hamjambo wananchi wa kilimanjarooooooo!!!!

Kwa mujibu wa taarifa ya mkoa wa Kilimanjaro, kesho atafungua mkutano wa mameya wa jiji, miji, wenyeviti na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, utakaofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha polisi mjini moshi.


Rais Kikwete (Katikati) ndani ya vazi la chama tawala na ishara ya chama(kidole gumba).

Katika ziara hii, Raisi anatarajiwa kufungua ofisi mpya za makao makuu ya jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro na baadae kuutembelea mradi wa kusambaza maji wa himo, sanjari na kugawa kadi kwa wanachama wapya wa CCM.

BRAZIL NA TAIFA STARS LEO




Hii ni bendera ya tanzania, nimeonyesha uzalendo kidogo.

Leo ni siku ambayo kila mtanzania mpenda soka na yule ambaye hapendi atakuwa makini kusikia matokeo ya mechi ambayo itachezwa usiku kati ya brazil. na taifa stars.

Mungu ibariki Taifa stars. Ameni!!!!!!!!!!!!!!!!!

MAENEO YA WAZI YAWA DAMPO KATA YA PASUA

Maeneo ya wazi katika kata ya pasua yamekuwa dampo baada ya kukosa sehemu maalumu ya kuweka taka wakati mpango wa ukusanyaji taka ukipingwa na wananchi.

Katika maeneo ambayo manispaa iliweka mankotena imekuwa ikilalamikiwa na wananchi haswa kutokuwepo kwa mankotena hayo na mengine kutoondolewa pindi yanapojaa takataka.

Moja kati ya eneo katika kata ya pasua ni eneo la wazi katika mtaa wa majengo mapya ambalo kwa sasa limekuwa eneo la kutupa taka na kuwa hatari ya milipuko ya magojwa. Eneo hili limenzungukwa na nyumba kitu ambacho ni hatari haswa kwa watoto wanaopenda kucheza eneo hilo




Hili ndio eneo la wazi la mtaa wa majengo mapya ambalo limekuwa sehemu ya kutupia taka (jalala).

Hii ni changamoto kwa viongozi husika kupambana na hali hii kuepuka na magojwa ya milipuko na maeneo haya ya wazi kubaki na kazi ambayo ndio lengo lake.

Think about it!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!





UFAGIO KWA WAFANYABIASHARA MOSHI

Mkutano wawaponza wafanyabiashara.

Mameya, wenyeviti na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya nchini,wanatarajiwa kukutana katika mkutano mkuu wa jumuiya ya Tawala zamikoa na serikali za mitaa-ALAT, unaokutana mjini Moshi Juni 9 hadi 10 mwaka huu.

Hali ya sasa moshi haswa katika maeneo yaliyozeeleka kwa wafanya biashara yamekuwa meupe. mfano mbele ya kituo cha polisi,kona ya mawenzi hospitali na karibu ya NMB bank ndio maeneo maarufu kwa wafanyabiashara wa viatu,soksi,mapazi,shuka na taulo.



Hali ndivyo inaonekana kwa sasa katika manispaa ya moshi.

Baadhi ya watu wamesema kuwa maeneo hayo huwa hayaruhusiwi kufanya biashara lakini kwa kipidi cha nyuma watu wamekuwa wakifanya biashara katika maeneo hayo. Hivyo basi, mkutano huu na Maneno ya Mkurugenzi wa halmashauri ya moshi ya kuweka mji safi inasemekana ni sababu ya mkutano huu.


Hili ni gari la halmashuri likiwa limemkamata Mfanyabiashara.

Hali ya jana kwa wanagambo walikuwa watendaji kwa kuwakamata na kuwakimbiza wafanyabiashara na bidhaaa zao. Hali hii imekuwa gumzo katika manispaa hii kwa wafanyabiashara kukaidi kwenda memorial(eneo ambalo limetengwa) kwa madai eneo hilo halina maandalizi na biashara bado ni changa.



Hawa ni wanamgambo wakimkimbiza mfanyabiashara wa viatu.

Ni changamoto kwa wahusika kulifanyia kazi ili kuachana na malumbano na wafanyabiashara haswa kwa kukaa pamoja na kufika muufaka. Maana hapa yapo mengi ya kujiuliza.

Ni hayo tu waungwana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.