Sunday, July 18, 2010

CHEKI SWAGGAZ ZA PROJECT 120!!!!!!!!!!!!

HOT PINDI NDANI YA MOSHI FM 90.2

Hii ni shoo kali ndani ya redio moshi fm kila ijumaa saa 7 hadi saa 10 jioni, wengi hawakosi kuisikiliza sikjui wewe. The big host wa hot pindi hili ni Mzeiiyaaaa wa milazo. Mzazi usijaribu kusikiliza hutaacha.


Nyie watoto kwa makamuzi si mchezo mnafanya balalaaaa. Huyu ni Ntoly Mayombole baada ya mzuka aliamua kuvamia shoo kwa upande wa pili wa studio.




Hisia za mziki zinapogusa mahala penyewe hakuna mkubwa wala mtoto, bosi wala mfanyakazi na milazo tata ni raha raha raha mpaka mwisho mwisho!!!!!!!!!!. Mwenye shati la drafti nyekundu na nyeupe ni Meneja wa redio moshi fm, Bw Deus Mworia.




Mwenye Tshirt ya mistari ya bluu na nyeupe(kushoto) ni Dj Poggo na mwenye tshirt nyekundu (kulia) ni Dj Q. Machizi ambao wanawakilisha vema katika shoo hii kali pia wagonga pini ndani ya club laliga


Mwenyewe headphone ni host wa hot pindi la project 120 Mzeiyaaa wa milazo na kwa mabli ni madj's wakigonga pini kwa ushirikiano.


The host wa hot pindi "project 120" Mzeiiiyaaaaaaaa akichongana na Dj Poggo.

Usiache kusikiliza Moshi Fm kwa vipindi vikali baada ya marekebisho ya nguvu.








HAPPY BIRTHDAY MADIBA!!!!!!!!!

HONGERA MANDELA MUNGU AKUZIDISHIE UMRI

Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela leo anatimiza miaka 92, huku ulimwengu ukisherehekea kwa mara ya kwanza, "Siku ya Nelson Mandela Duniani" kwa heshima ya kiongozi huyo.


Viongozi wa kimataifa na watu wa kawaida nchini Afrika Kusini na nje ya nchi hiyo, wameahidi kujitolea kuhudumia jamii kwa dakika 67 katika ishara za kuadhimisha miaka 67 ya kiongozi huyo kushughulikia kisiasa.
Tangu kuondoka madarakani, Mandela amejitokeza hadharani mara chache tu. Juma lililopita alikwenda kwenye uwanja wa michezo wa Soccer City mjini Johannesburg, kuwapungia mkono mashabiki wa kandanda kabla ya kufunguliwa mchezo wa fainali wa Kombe la Dunia, lakini hakubakia kutazama mchezo kwa sababu ya hali yake dhaifu ya afya.

Tuesday, June 22, 2010

AFRIKA BYE BYEEEEEEEEEEEEE!!!!!!!!!!!!!!!!!!


Wenyeji wa kombe la dunia, Afrika Kusini wametupwa nje ya fainali za kombe la dunia pamoja na kwamba walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ufaransa katika mechi yao ya mwisho.
Hata hivyo Vigogo wa ulaya Ufaransa wameliaga kombe la dunia wakishika mkia kwenye kundi baada ya Afrika Kusini kuwabebesha virago.
Wawakilishi wengine wa Afrika, Nigeria watabidi wajilaumu wenyewe kwa kuliaga mapema kombe la dunia, kutokana na nafasi nyingi za wazi walizozipoteza.
Nigeria ilihitaji ushindi kwenye mechi yake dhidi ya Korea Kusini, lakini iliambulia sare ya magoli 2-2, yalifungwa na Kalu Uche kwenye dakika ya 12 na Yakubu kwa njia ya penalti kwenye dakika ya 69.
Matumaini ya Afrika yamebaki kwa timu za Algeria, Ghana na Ivory Coast.

Monday, June 21, 2010

CAMEROON BYE BYEEEEEEE!!

Cameroon timu ambayo ilikuwa miongoni mwa timu zilizokuwa zikitajwa kama “tumaini la Afrika”,imeyaaga mashindano hayo baada ya kufungwa jumla ya magoli 2-1 na Denimark


Timu hiyo imebakiza mechi moja kwa heshima ya michezo ingawa kushinda si sababu ya kuendelea bali kujiwekea sifa nzuri kiduchu ila kufungwa ni aibu ambayo itakuwa na historia kwa timu hiyo kubwa.

Mchezaji mkali Eto alisadikika ni kati ya wachezaji ambao watacheka na nyavu ingawa amecheka na nyavu mara moja.

Poleeeeni ndio michezo.!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

RAIS KIKWETW ACHUKUA FOMU YA URAIS

Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya M. Kikwete, Leo mchana amechukua fomu ya kutetea kiti chake cha uraisi kupitia chama cha mapinduzi huko mkoani dodoma.

Kikwete anakuwa mwanachama wa kwanza kuchukua fomu za kuwania kiti cha uraisi, uchaguzi utakaofanyika oktoba mwaka huu.

Akikabidhiwa fomu na Katibu mkuu wa chama hicho Yusuph Makamba, kuliambatana na sherehe za kumpongeza huku wana CCM wakijitokeza kwa ajili ya kumdhamini.


Kikwete akikabidhiwa fumu na Makamba!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!