Akifafanua zaidi amesema kuwa mwanzoni kabisa wakianza game kulikuwa hamna bongo fleva ila walikuwa wanafanya hip hop (michano) ndio maana ukiuliza hip hop lazima utaje arusha.

Akihojiwa na Kituo kimoja cha Television nchini JCB amesema kuwa bongo hip hop ni mziki unaoeleza hali halisi ya kitaa yaani maisha kwa ujumla si bongo fleva mziki wa kusemana.
Akielezea malengo yake amesema kuwa sasa hivi ameamua kusimamam mwenyewe baada ya kutoa album tatu za kundi la Watengwa kama Iliandikwa, Fulu ile laana na Piga takatifu.
JCB amelonga kuwa yupo kwenye maandalizi ya kumalizia album yake ndani ya bongo (DSM) katika studio za Mj na Tongwa Records kwa ajili ya kufanyia mastering.
Aidha amesema album hiyo ina nyimbo 16 na bado yupo katika mchakato wa kutafuta jina baada ya kupata majina mawili “Makala ya makala na Kijiti” ili kuchagua ni jina ambalo litakuwa mzuka.
Ni hayo tu toka R-chuga.
No comments:
Post a Comment