Saturday, June 12, 2010

JON B APANIA KUWAPANDISHA WASANII WA KASKAZINI

Produza Jon B anayepiga mzigo pande za R-chuga "Arusha" chini ya studio ya Grandmasters records amesema wasanii wa kanda ya kaskazini wana kila sababu ya kuhakikisha wanafanikiwa kutoka ingawa nguvu bado ni ndogo miongoni mwa wadau wa mziki huu wa kizazi kipya.

Akiongea na blog hii ya kitaa kwa ufahamu zaidi amesema kuwa wapo wasanii wenye uwezo na wanafanya vizuri lakini bado kanda ya kaskazini hatuna mtandao wa umoja kati ya wasanii, watangazaji, maproduza na wadau wa mziki.


Jon B

"Kitu muhimu ni kuwa na network itayotufanya tufahamiane vizuri na endapo kna jambo tunataka kulifanya basi tutashirikiana na kulifanikisha,ndio maana nimenzaa kukutfahumu wewe Wamilazo na wewe umenifahamu na nitaendelea kufahamiana na wengine. Alisema Jon B

Jon B ambaye pia aligusia wasanii wa kaskazini ambao wapo bongo, amesema haina haja leo hii ya kutoka huku kwetu na kwenda bongo wakati tuna uwezo ila tatizo ni sisi kutokuwa na mtandao wa kuhakikisha tunafahamiana na kusaidiana na kuwashawishi wengine haswa wasanii wenye majina kuja moshi kufanya kazi na kuchezwa.

Aidha, amesema kuwa kwa sasa tayari amefanya kazi kibao ambazo anatarajia kuziachia hivi karibuni na pia alikuwa katika mchakato wa kumalizia album ya John Walker na Ras Lion inayoitwa Sumu ya Panya kwa ajili ya kwenda sokoni.

Ni hayo tu toka R-chuga........................................................................................

No comments:

Post a Comment