Monday, June 14, 2010

Vijana Vyuo Vikuu Dodoma Waandamana kumuunga mkono Rais Kikwete kugombea Urais kwa tiketi ya CCM Mwaka huu!!

Mwenyekiti wa CCM taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaongoza wanachama wapya wa CCM kula kiapo cha utii kwa Chama Cha Mapinduzi muda mfupi baada ya kuwakabidhi kadi za uanachama wakati wa maandamano ya kumuunga mkono yaliyofanyika mjini Dodoma.


Baadhi ya vijana kutoka vyuo vikuu mbalimbali mjini Dodoma wakiandamana kumuunga mkono Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuchukua fomku kwaajili ya kugombea nafasi ya urais 2010.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika vyuo vikuu mbalimbali mjini Dodoma walishiriki katika maandamano ya kumuunga mkono kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi ya Urais mwaka huu kwa tiketi ya CCM.

Vijana wengine mpo wapi na vyama vyenu au hamuwapendi viongozi wenu wa taifa?

No comments:

Post a Comment