Saturday, June 12, 2010

UMESHAWAHI KUCHEZA MCHEZO HUU

Maisha siku zote huwa tofauti toka ulipokuwa mtoto hadi kfikia uzeeni. Hatua hii hupitia mambo mbalimbali haswa za kimechozo. Nakumbuka nikiwa mtoto tulicheza michezo mingi ya heshima tofauti na watoto wa sasa hivi ambapo usipokuwa makini wewe mzazi, mchezo wao ni ule wa baba na mama (kujenga magofa). Haya yote yanasemekana ni kutokana na utandawazi ambao huwajengea watoto ufahamu zaidi.


Huu ni mchezo wa Kuruka kamba ambao tuliucheza utotoni na pia kiafya una umuhimu. Michezo mingine ni Tikiri, Kombolele(Mchezo wa kujificha), Utengenezaji wa magari, Ndege wakati wa mavuno, Midoli ya kutengeneza, Kuendesha treli kwa kutumia betri ukiwa umechimba kijimtaro chiniKula mbakishie baba, Kuteneneza vitu mbalimbali kwa kutumia udongo, ukutiukuti,Kioo Kioo,Nage,Kujipikilisha....................................
Mingine nisaidie uzeee,nimesahau......!!!!!!!!

Tafakai juu ya mtoto wako ingawa sasa hivi tunaishi kizungu tunawanunulia vitu vya kuchezea ila wanavitumia ipasavyo au wanachunguzana miiili yao?....

No comments:

Post a Comment