Saturday, June 12, 2010

UMEME KUKATIKA TANZANIA SIKU TATU

SHIRIKA la umeme nchini (Tanesco), limesema maeneo kadhaa katika mikoa 11 nchini yatakosa umeme kwa muda wa siku tatu kuanzia leo.

Mikoa hiyo ni Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga, Mbeya, Morogoro, Tabora, Mara, Singida na Tanga.

Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud amesema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hitilafu iliyotokea katika mitambo ya Songas na kidatu, tatizo ambalo lipo nje ya uwezo wa shirika lake licha ya wataalamu kujitahidi kukabiliana na hali ili kuwapatia umeme wateja wake; hasa wakati huu wa michuano ya Kombe la Dunia inyaofanyika Afrika Kusini.

"Katizo hilo litakuwepo kuanzia Juni 12 -15, mwaka huu kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 5:00 usiku," alieleza Masoud katika hiyo.

No comments:

Post a Comment