Friday, June 11, 2010

TMK WANAUME YAVUNJIKA

Wasanii waliotengwa katika kundi la TMK wanaume halisi baada ya kuchaguliwa wasanii watano na Sir Nature watakaowakilisha kundi hilo wameamua kuanzisha kundi lao linalojulikana kwa jina la Wanaume.

Kampuni ya Mpo Afrika imetangaza kusaini mkataba na kundi jipya, likiundwa na wanamuziki kama Athuman Yahya (A.Man), Juma Mbelwa (Juma Jazz), Karim Kaiman (Kakaman), Abdul Ally (Mzimu), Richard Shauri (Rich One) pamoja na David Mpangile (Daz-p) walioachwa katika kundi la TMK Wanaume Halisi.


WAHUSIKA WALIOTENGENEZA KUNDI LA WANAUME

Hassan Umande amesema lengo la kuunda kundi hilo jipya ni kwa ajili ya kuendeleza sanaa na kuleta mabadiliko katika anga ya muziki wa kizazi kipya aka bongofleva hapa nchini.

Aidha ameongezea kuwa kuna vikwazo vingi vilivyotokea mpaka kuamua kujitenga ,yote hiyo kuepuka migongano ambayo kimsingi si ya lazima kwa sababu sote ni vijana na tunatafuta maisha,kwa hiyo kwa sababu tumetengwa basi tumeamua kuunda kundi la watu sita.

NI HAYO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment