Monday, June 7, 2010

TAIFA STARS 1 - BRAZIL 5

Timu ya taifa ya Tanzania, Taif Stars, imepaia kichapo cha magoli 5-1 katika mechi ya kujipima nguvu iliyofanyika Jana jioni katika uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.

Mshambuliaji Robinho ndiyo aliwapatia Brazil goli la kwanza, kabla ya kuongeza la pili kwenye mechi ambayo si makosa kusema Taifa Stars walicheza vizuri ingawa tatizo la kawaida limekuwa likijirudia - kukosekana kwa maarifa ya kufunga.


Kaka akitoa dole tu......!!!!

Shambulio la Kaka na mengine mawili kutoka kwa mchezaji wa akiba, Ramires yalikamilisha magoli kwa The Selecao, lakini Stars walionekana kuwachokoza Brazil ambapo katika dakika ya sita Mrisho Ngassa alikosa goli la wazi.

Taifa Stars walipata goli la kufutia machozi kupitia Jabir Aziz, mchezaji wa akiba aliyemalizia kwa kichwa mpira wa kona.

Mchezaji muhimu aliyekosekana ni mlinda mlango namba moja Julio Cesar aliyejeruhiwa katika mechi ya majaribio dhidi ya Zimbabwe juma lililotangulia, badala yake alicheza mlangoni alicheza Heurelho Gomes.

Tukaze buti tutaweza................................................

No comments:

Post a Comment